Jumamosi, 7 Novemba 2015

Magufuli afanya ziara ya kushtukiza Wizara ya Fedha!


Umbali wa takribani kilomita moja kutoka ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais mpya wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli. Rais anatembea hadi Wizara ya Fedha anapowakuta ‘wazembe’ wakiwa nje ya ofisi.
Tukio hilo la jana lilikuwa la kushtukiza, lisilotarajiwa na wakazi wa jijini kumuona Rais Magufuli akiwa katika siku ya pili ya utawala wake, ‘akikatiza’ kwa mguu kwenda wizarani hapo.
Akiwa katika kampeni na baada ya kutangazwa mshindi wa kiti cha urais, Rais Magufuli aliwaonya watumishi wa umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea na uzembe na wasioweza mabadiliko, waanze kuondoka.
Akiwa katika kuthibitisha kauli mbiu yake ya ‘hapa ni kazi tu’, Rais Magufuli aliingia wizarani hapo na kukuta baadhi ya viti sita vikiwa wazi, taarifa ikaeleza kwamba watumishi wahusika walikuwa nje ya ofisi kunywa chai.
Ili kupata ushahidi usiotiliwa shaka, Rais Magufuli alishika kiti kimoja baada ya kingine, akiuliza jina la mtumishi anayekitumia na mahali alipo.
Rais mpya wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli amefanya ziara hiyo fupi kutoka ikulu muda mfupi baada ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu George Mcheche Masaju.  
Bw Masaju aliteuliwa mara ya kwanza kuwa Mwanasheria Mkuu na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Januari mwaka 2015, baada ya kujiuzulu kwa George Werema.Rais  Magufuli hakuzungumza rasmi na wanahabari baada ya kumaliza ziara hiyo. 
Hata hivyo, mwandishi wa www.arcuyo.blogspot.com Paskal Linda  anasema kuna uwezekano amezungumza na maafisa wa hazina kuu kuhusu hali ya mikopo ya wanafunzi. Wakati wa kampeni, Rais John Magufuli aliahidi kufanya elimu kuwa bila malipo kuanzia shule za msingi hadi shule za sekondari. 
 
Picha juu Mwanasheria Mkuu George Mcheche Masaju.  

Taarifa kutoka ikulu ya Dar es Salaam zinasema kwenye mkutano na maafisa wakuu wa Wizara ya Fedha, Rais Magufuli aliwaagiza kuziba mianya yote inayotumiwa na wakwepa kodi. Rais Magufuli ameagiza Bunge lifunguliwe Novemba 17 na anatarajia kuwasilisha jina la Waziri Mkuu wake kwa bunge hilo Novemba 19.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni