Tudumishe utamaduni wetu:

 Mdada akichunja pombe ya asili, na hivyo ndivyo walivyofanya hapo kale na pia kuna baadhi ya sehemu Afrika bado inafanyika  hivyo

Na hapa ni nyumba ya asili huko Afrika ya kusini/ hasa kwa kabila la kizulu. Ambao inasemekana ni wanaukoo na wangoni.
Na hapa ni nyumba ya asili ya wangoni iliyopo Songea  pale Makumbusho ya Mashujua

Ramani ya bara la Afrika
 Moja ya sanaa za Kiafrika

Rais Jakaya Kikwete akipiga ngoma ya kisukuma, 

moja ya tamadauni za Kitanzania 
 Kingo, moja ya majarida ya Kitanzania. 
Hapa alikuwa akitafuta Miss Tanzania wa ukweli

  
 Ujumbe kutoka Chama cha Sanaa na Fasihi cha China 
ukiangalia vinyago mjini Dar es salaam
 watemi wa kisukuma wakiwa katika vazi asili la wasukuma
vijana wakisukuma wakiwa katika vazi la ngoma za kisukuma maarufu kwa jina la ngoma.  Hapa Maria Nyanjige akielezea mfano wa ngoma hii iliyotumika wakati Chifu wa kisukuma anaoa, anasimikwa kuwa chifu au akiwa amefariki dunia ngoma hii ilipigwa katika matukio kama hayoHii ni nyumba iliyohifadhi ngoma hizo zinazopigwa wakati chifu wa kisukuma anapokuwa na matukio muhimu lakini pia ni mfano wa kiti anachokalia chifu wa kisukuma kama unavyoiona huku chini.Hili ni bao amalo lilitumiwa na machifu kushindana, kwa mfano wao walikuwa hawapigi kura wakati wakichagua kiongozi wa eneo lao , ila machifu hao walitumia bao kushindania madaraka na aliyemfunga mwenzake kete nyingi ndiye aliyetawazwa kuwa chifu wa eneo fulani. Hii ni ramani inayoonyesha majimbo yao ambayo machifu walitawala katika kipindi hicho.Huu ni mwamba uliotumika kusaga nafaka mbalimbali katika familia ya chifu na ilikuwa ni lazioma uwepo katika eneo la makazi ya chifu ikiwa ni pamoja na Zizi la Ng”ombe, Mti mkubwa kwa ajili ya kuvuli, Mawe kwa ajili ya kusaga dawa, ghala ya kuhifadhia nafaka kiota kikubwa kwa ajili ya kuhifadhia kuku na sehemu maalum ya tambiko la KisukumaHuu ni mfano wa eneo lilitumika kwa kufanya maombi ya kimila na kufanya toba kama kuna madhambi wamefanya, kabla ya wazungu na waarabu kuleta dini zao.Michuzijunior mkurugenzi wa JIACHIE kushoto akiwa na Maria Nyanjige Mhifadhi Msaidizi wa Makumbusho ya Bujora mbele ya nyumba illiyohifadhi vifaa mbalimbali vilivyotumika kwa ajili ya michezo ya kabila la Kisukuma Bagika na Bagalu, yaani utamaduni uliokuwa na ushindani mkubwa kama vile Simba na Yanga.Hii ni nyumba maalum ambayo ilitumika kuhifadhia madawa, na vifaa mbalimbali kwa ajili ya kufanyia tiba ya kiasili.Hili ni ghala ambalo lilitumika kuhifadhia chakula  na mpaka leo ghara hili hutumika katika familiahttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-8dFVMA7saF-c2EvH03nqcaoyED3f3hkpVAlSNFKBJX3iWHOFDMUNfStor6UZ708ckavWwgB0gLTFgIMJ6zYxbbo6rlTFcLelcWWLtxAKBVeOfV51AtS4OnEjEZ6W2_UZy_y_9i5txUKP/s400/5.jpg
Hivi ni vifaa vilivyotumika katika shughuli za uhunzi,natumaini msomaji wa blog yangu utakua umeelewa mengi kuhusu kabila la wasukuma.

Charles Madatta kwa niaba ya Fabian Mhoja ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Makumbusho hayo akionyesha nyumba walizokuwa wakiishi wasukuma.


Moja ya nyumba ambazo zilikuwa zikitumia na wafalme wa Kisukuma kwa ajili ya kukutana na kucheza ngoma za asili ya  kisukuma.

Maoni 1 :